Home

Kutoka Bungeni: Sugu anajibu tuhuma za kupora mtoto kutoka kwa mzazi mwenzake

03:37


  1. Baada ya jana Martha Mlata
    kumtuhumu Sugu kumpora mtoto 
    toka kwa mama yake. 
    amemuomba Spika kutoa maelezo binafsi. 
    Kwanza anakiri mtoto ni wake, 
    na anasema watu wazima 
    hawazungumzii mambo ya ndoa za wenzake 
    na anasema ni mambo binafsi.


    Anasema binti yake ameishi Dar
    tangu mwaka 2012 
    na amekuwa akilipa laki tano kila mwezi 
    na mi 3 kwa mwaka kama karo.

    Anasema mzazi mwenzake amekuwa 
    akivaa nusu uchi na 

    kuachasehemu za siri nje.
    Anasema Mlata anayejiita mlokole 
    hawezi kutetea maovu kama hayo, 
    na yeye hasemi kwa nini ndoa yake 

    ilivunjika .
    Anasema kile kinachodaiwa kuwa 
    kumpora mtoto ni hukumu ya mahakama
    na Mlata hakuwa shaidi wala hana uhakika 

    kama hata mtoto mwenyewe anamjua.

    Anasema kwa kuwa ni mambo ya faragha 
    hata Mlata asingetaka mambo 

    yake na mabwana zake wa sasa yajulikane.

    Anasema hata mtoto hajamchukua 
    na ameacha maswala ya kifamilia 

    yachukue mkondo wake.

    Ndugai anasema suala hili liachwe 
    maana linaweza kumuathiri mtoto 
    kisaikolojia hata shule.
    Anawataka waandishi wa habari kuliacha suala hili.  
    MH. J. mbilinyi
    Sugu anatokwa na machozi kwa uchungu

Home

POLISI WASHUTUMIWA AFRIKA KUSINI

22:48

Polisi washutumiwa Afrika kusini

Polisi wamekuwa wakitoa utetezi wao kuwa walikuwa wanajihami
Tume ya uchunguzi nchini Afrika kusini imetaka ufanyike uchunguzi dhidi ya Polisi kuhusu mauaji ya wafanyakazi 34 wa mgodi yaliyofanyika mwaka 2012.
Rais wa nchi hiyo, Jacob Zuma amesema uchunguzi umebaini kuwa Polisi walikuwa na mpango usiofaa kumaliza mgomo katika mgodi mgodi wa Marikana na ilikuwa makosa kuutekeleza.
Wakati wote Polisi wamekuwa wakidai kuwa walikuwa wakijihami wakati wa mgomo wa wafanyakazi waliokuwa wakidai kuongezwa kwa mishahara.
Rais Zuma ameliita tukio hilo kuwa baya na kusema kuwa halina nafasi katika Demokrasia ya nchi hiyo.
Mauaji ya Marikana yanaelezwa kuwa mabaya kutokea nchini Afrika kusini tangu baada ya kumalizika kwa ubaguzi wa rangi miaka 20 iliyopita.
Wafanyakazi wa mgodi waligoma kwa siku kadhaa,na watu 10 tayari walipoteza maisha wakiwemo watu ambao hawakuwa kwenye mgomo, walinzi wa mgodi na Polisi, kabla ya tukio la tarehe 16 Agosti

Like us on Facebook

About me

Ismail mbaazi
Email: mbaazishumaa6@gmail.com
#+25565-9230-273